Saturday, October 22, 2016
Wednesday, October 19, 2016
Chombo cha anga za juu cha Ulaya kutua Mars
Chombo cha anga za juu cha Ulaya Schiaparelli
kimefanikiwa kujitenga na "chombo mama" angani
na kwa sasa kinaelekea kwenye sayari ya Mars.
Chombo hicho kinatarajiwa kujaribu kutua kwenye
sayari hiyo Jumatano.
Chombo hicho cha uzani wa kilo 577 kilifanikiwa
kujitenganisha na chombo mama Jumapili saa
14:42 GMT (saa kumi na moja jioni saa za Afrika
Mashariki).
Mpango wa kupeleka watu wakaishi Mars
Mpango wa Marekani kupeleka watu Mars
Chombo hicho kitakuwa na muda wa chini ya
dakika sita kupunguza kasi yake ya kilomita
21,000 kwa saa kiasi cha kukiwezesha kutua
salama kwenye sayari hiyo.
Schiaparelli ni kifaa cha kufanyia majaribio
teknolojia, na lengo kuu ni kudhihirisha uwezo wa
Shirika la Anga za Juu la Ulaya (ESA) kutua katika
sayari hiyo.
Jaribio la awali la shirika hilo kutua katika sayari
hiyo lilifanyika mwaka 2003, kwa kutumia chombo
cha Uingereza cha Beagle-2.
Chombo hicho kilifanikiwa kutua salama lakini
kikashindwa kufungua mitambo yake ya kawi ya
jua vyema na hivyo mawasiliano yakakatika.
Chombo hicho kikifanikiwa kutua salama,
kitatumiwa kufanya uchunguzi kwenye sayari hiyo.
kimefanikiwa kujitenga na "chombo mama" angani
na kwa sasa kinaelekea kwenye sayari ya Mars.
Chombo hicho kinatarajiwa kujaribu kutua kwenye
sayari hiyo Jumatano.
Chombo hicho cha uzani wa kilo 577 kilifanikiwa
kujitenganisha na chombo mama Jumapili saa
14:42 GMT (saa kumi na moja jioni saa za Afrika
Mashariki).
Mpango wa kupeleka watu wakaishi Mars
Mpango wa Marekani kupeleka watu Mars
Chombo hicho kitakuwa na muda wa chini ya
dakika sita kupunguza kasi yake ya kilomita
21,000 kwa saa kiasi cha kukiwezesha kutua
salama kwenye sayari hiyo.
Schiaparelli ni kifaa cha kufanyia majaribio
teknolojia, na lengo kuu ni kudhihirisha uwezo wa
Shirika la Anga za Juu la Ulaya (ESA) kutua katika
sayari hiyo.
Jaribio la awali la shirika hilo kutua katika sayari
hiyo lilifanyika mwaka 2003, kwa kutumia chombo
cha Uingereza cha Beagle-2.
Chombo hicho kilifanikiwa kutua salama lakini
kikashindwa kufungua mitambo yake ya kawi ya
jua vyema na hivyo mawasiliano yakakatika.
Chombo hicho kikifanikiwa kutua salama,
kitatumiwa kufanya uchunguzi kwenye sayari hiyo.
Leicester City yang'ara UEFA
Klabu ya soka ya Leicester City imeendeleza wimbi
la ushindi katika michuano ya ligi ya mabingwa
barani Ulaya baada ya kuibuka na ushindi wa bao
1-0 dhidi ya FC Copenhagen.
Wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani King
Power, Leicester walipata bao hilo dakika tano
kabla ya kwenda mapumzikoni kupitia kwa Riyad
Mahrez aliyekuwa katika kiwango cha hali ya juu
baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Mualgeria
mwenzake Islam Slimani.
Kwa matokeo hayo Leicester wanabaki kileleni
mwa kundi G wakiwa na alama 9 baada ya
kushinda michezo yote mitatu ya ufnguzi wa ligi
ya mabingwa Ulaya.
Timu pekee zilizowahi kushinda michezo mitatu ya
ufunguzi katika michuano hiyo ni AC Milan, Paris
St-Germain, Juventus na Malaga.
Matokeo mengine ya Ligi ya mabingwa barani
Ulaya
Bayer 04 Leverkusen 0-0 Tottenham Hotspur F.C.
CSKA Moscow 1-1 AS Monaco FC
Real Madrid 5-1 Legia Warsaw
Sporting 1 -2 Borussia Dortmund
Club Brugge 1-2 FC Porto
Dinamo Zagreb 0- 1 Sevilla
Lyon 0- 1 Juventus
la ushindi katika michuano ya ligi ya mabingwa
barani Ulaya baada ya kuibuka na ushindi wa bao
1-0 dhidi ya FC Copenhagen.
Wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani King
Power, Leicester walipata bao hilo dakika tano
kabla ya kwenda mapumzikoni kupitia kwa Riyad
Mahrez aliyekuwa katika kiwango cha hali ya juu
baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Mualgeria
mwenzake Islam Slimani.
Kwa matokeo hayo Leicester wanabaki kileleni
mwa kundi G wakiwa na alama 9 baada ya
kushinda michezo yote mitatu ya ufnguzi wa ligi
ya mabingwa Ulaya.
Timu pekee zilizowahi kushinda michezo mitatu ya
ufunguzi katika michuano hiyo ni AC Milan, Paris
St-Germain, Juventus na Malaga.
Matokeo mengine ya Ligi ya mabingwa barani
Ulaya
Bayer 04 Leverkusen 0-0 Tottenham Hotspur F.C.
CSKA Moscow 1-1 AS Monaco FC
Real Madrid 5-1 Legia Warsaw
Sporting 1 -2 Borussia Dortmund
Club Brugge 1-2 FC Porto
Dinamo Zagreb 0- 1 Sevilla
Lyon 0- 1 Juventus
Tuesday, October 18, 2016
Wanasayansi kuundwa taifa jipya anga za juu
Kundi la wanasayansi mjini Vienna, Austria
wameanzisha mpango wa kuunda taifa la amani la
aina yake ambalo litakuwa na jina Asgardia.
Taifa hilo litaundwa katika anga za juu, eneo.
Maelezo kwenye tovuti ya wanasayansi hao
yanasema taifa hilo litakuwa nje ya udhibiti wa
mataifa yoyote ya sasa na litakuwa katika mzingo
wa dunia, eneo ambalo vyombo vya anga za juu
huzunguka dunia.
Wanasayansi hao wanapanga kurusha satelaiti ya
kwanza, ya kuanzisha taifa hilo, mwishoni mwa
mwaka ujao.
Mpango wa kupeleka watu wakaishi Mars
China yatuma wataalamu mzingo wa dunia
Matumaini ya wataalamu hao ni kwamba siku moja
hivi karibuni watatambuliwa na Umoja wa Mataifa.
Lakini baadhi ya wataalamu wanatilia shaka
uwezekano wa mpango huo kufanikiwa ikizingatiwa
kwamba sheria za kimataifa huzuia mataifa kudai
umiliki wa maeneo anga za juu.
"Raia" wa Asgardia, ambao watachunguzwa kwa
makini kabla ya kukubaliwa, mwishowe watapewa
hata pasipoti, anasema Lena de Winne, mmoja wa
maafisa wakuu wa mradi huo ambaye alifanya kazi
kwa miaka 15 katika Shirika la Anga za Juu la
Ulaya (EPA).
Mradi huo unaongozwa na shirika la Aerospace
International Research Center, ambalo lilianzishwa
na mwanasayansi Mrusi, ambaye pia ni
mfanyabiashara, Dkt Igor Ashurbeiyli.
Mashindano yanaandaliwa kuamua bendera na
wimbo wa taifa wa nchi hiyo mpya.
Profesa Sa'id Mosteshar, mkurugenzi wa Taasisi ya
Sera na Sheria za Anga za Juu ya London,
amesema itakuwa vigumu kwa Asgardia
kutambuliwa kama taifa ikizingatiwa kwamba
haitahusiana na taifa lolote linalojitawala duniani,
na pia 'raia wake' wengi watakuwa ardhini.
Tayari zaidi ya watu 50,000 wamewasilisha
maombi mtandaoni kutaka kuwa raia wa taifa hilo.j
wameanzisha mpango wa kuunda taifa la amani la
aina yake ambalo litakuwa na jina Asgardia.
Taifa hilo litaundwa katika anga za juu, eneo.
Maelezo kwenye tovuti ya wanasayansi hao
yanasema taifa hilo litakuwa nje ya udhibiti wa
mataifa yoyote ya sasa na litakuwa katika mzingo
wa dunia, eneo ambalo vyombo vya anga za juu
huzunguka dunia.
Wanasayansi hao wanapanga kurusha satelaiti ya
kwanza, ya kuanzisha taifa hilo, mwishoni mwa
mwaka ujao.
Mpango wa kupeleka watu wakaishi Mars
China yatuma wataalamu mzingo wa dunia
Matumaini ya wataalamu hao ni kwamba siku moja
hivi karibuni watatambuliwa na Umoja wa Mataifa.
Lakini baadhi ya wataalamu wanatilia shaka
uwezekano wa mpango huo kufanikiwa ikizingatiwa
kwamba sheria za kimataifa huzuia mataifa kudai
umiliki wa maeneo anga za juu.
"Raia" wa Asgardia, ambao watachunguzwa kwa
makini kabla ya kukubaliwa, mwishowe watapewa
hata pasipoti, anasema Lena de Winne, mmoja wa
maafisa wakuu wa mradi huo ambaye alifanya kazi
kwa miaka 15 katika Shirika la Anga za Juu la
Ulaya (EPA).
Mradi huo unaongozwa na shirika la Aerospace
International Research Center, ambalo lilianzishwa
na mwanasayansi Mrusi, ambaye pia ni
mfanyabiashara, Dkt Igor Ashurbeiyli.
Mashindano yanaandaliwa kuamua bendera na
wimbo wa taifa wa nchi hiyo mpya.
Profesa Sa'id Mosteshar, mkurugenzi wa Taasisi ya
Sera na Sheria za Anga za Juu ya London,
amesema itakuwa vigumu kwa Asgardia
kutambuliwa kama taifa ikizingatiwa kwamba
haitahusiana na taifa lolote linalojitawala duniani,
na pia 'raia wake' wengi watakuwa ardhini.
Tayari zaidi ya watu 50,000 wamewasilisha
maombi mtandaoni kutaka kuwa raia wa taifa hilo.j
Diamond na Harmonize washinda tuzo Marekani
Afrika Mashariki imekuwa na furaha kubwa wikendi
kwenye tuzo za kila mwaka za Jarida la mziki
Afrika, maarufu kama Afrimma Awards baada ya
wasanii wa Kenya na Tanzania kuzoa tuzo tofauti
kwenye hafla iliyofanyika Marekani wikendi.
Imekuwa ni ushindi mkubwa kwa Wasanii wa lebo
ya Wasafi kutoka Tanzania, Diamond Platnumz na
Harmonize walioibuka mabingwa kwenye vitengo
vyao.
Diamond alimshinda Mtanzania mwenzake, Ali Kiba
katika kitengo cha mwanamuziki bora wa kiume
Afrika Mashariki.
Harmonize, anayezidi kuvuma kwa wimbo wake wa
'Inde' aliomujmuisha Dully Sykes, akitunukiwa tuzo
ya Msanii mpya wa mwaka.
Diamond Platinumz: Usitosheke kuvuma
nyumbani pekee
Hata hivyo Diamond hakuweza kuhifadhi taji lake
la msanii bora wa mwaka aliloshinda mwaka wa
2015 kwani tuzo hiyo ilikwenda kwa Mnigeria
Falvour.
Kwa upande mwingine, Kenya ilipata tuzo tatu
kupitia Msanii wa nyimbo za injili, Willy Paul,
aliyeshinda kitengo cha msanii bora wa injili nalo
kundi la Sauti Soul likapewa tuzo ya kundi bora la
mwaka.
Mwanamuziki wa kike, Akothee, aliondoka na taji la
mwimbaji bora wa kike licha ya mashabiki kutishia
kutompigia kura.f
kwenye tuzo za kila mwaka za Jarida la mziki
Afrika, maarufu kama Afrimma Awards baada ya
wasanii wa Kenya na Tanzania kuzoa tuzo tofauti
kwenye hafla iliyofanyika Marekani wikendi.
Imekuwa ni ushindi mkubwa kwa Wasanii wa lebo
ya Wasafi kutoka Tanzania, Diamond Platnumz na
Harmonize walioibuka mabingwa kwenye vitengo
vyao.
Diamond alimshinda Mtanzania mwenzake, Ali Kiba
katika kitengo cha mwanamuziki bora wa kiume
Afrika Mashariki.
Harmonize, anayezidi kuvuma kwa wimbo wake wa
'Inde' aliomujmuisha Dully Sykes, akitunukiwa tuzo
ya Msanii mpya wa mwaka.
Diamond Platinumz: Usitosheke kuvuma
nyumbani pekee
Hata hivyo Diamond hakuweza kuhifadhi taji lake
la msanii bora wa mwaka aliloshinda mwaka wa
2015 kwani tuzo hiyo ilikwenda kwa Mnigeria
Falvour.
Kwa upande mwingine, Kenya ilipata tuzo tatu
kupitia Msanii wa nyimbo za injili, Willy Paul,
aliyeshinda kitengo cha msanii bora wa injili nalo
kundi la Sauti Soul likapewa tuzo ya kundi bora la
mwaka.
Mwanamuziki wa kike, Akothee, aliondoka na taji la
mwimbaji bora wa kike licha ya mashabiki kutishia
kutompigia kura.f
Subscribe to:
Posts (Atom)